Uambishaji



Neno uambishaji linatokana na kitenzi kuambisha ambalo nalo latokana na kitenzi kuamba. Kuamba maana yake ni kukifunga kitu fulani kwenye kitu kingine ili kibakie hapo; au kukinatisha kitu fulani kwenye kitu kingine. Neno kuambisha lina maana ya kukifanya kitu kinate mahali fulani.  

Katika Kiswahili, uambishaji unafanyika kwa kuongeza mofu fulani mwanzoni au mwishoni mwa mzizi wa neno. Kwa mantiki hii, maneno yanayoundwa hupewa maana ama mpya, au ya ziada au hata yakageuza hali yake ya asili na kuchukua nafasi nyingine katika muundo wa kishazi. Kinachoambishwa huitwa kiambishi ambacho, aghalabu, hubeba maana katika lugha; na kwa mantiki hiyo, kiambishi ni sawa na mofu.

Kwa mfano, katika neno piga, pig ni mzizi, na a ni kiambishi/mofu ishilizi au tamatishi katika kila kitenzi asilia cha Kiswahili.           
           
Tunaweza kunatisha viambishi kadhaa mwanzoni mwa mzizi pig kama ifuatavyo:
           
            tu-ta-m-pig - a,

lakini pia tunaweza kunatisha viambishi kadhaa mwishoni mwa mzizi uo huo pig kama ifuatavyo:
                 
            pig-an-ish-a

au hata pengine tunaweza kuvinatisha viambishi vya mwanzoni na vya mwishoni mwishoni mwa mzizi huo huo pig na kupata tungo kama ifuatavyo:

            tu-ta-m- pig -an-ish-a; au

            tu-ta-m-pig - an-ish-a-je ?  (na wenzake).
Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment