TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI



Fasihi Simulizi
Fasihi Andishi
a)
Umri: Ina umri mkubwa kuliko fasihi andishi.  Pengine huitwa fasihi kongwe.
Ina umri mfupi kuliko fasihi simulizi. Hii inatokana na ukweli kuwa maandishi yamegunduliwa hivi karibuni.
b)
Uhifadhi: Inahifadhiwa kwa kichwa na kusambazwa kwa njia ya masimulizi.
Inahifadhiwa kwa maandishi na kusambazwa kwa njia ya maandishi.
c)
Tanzu: Ina tanzu mbalimbali, lakini ni tanzu nyingi kuliko zile za fasihi andishi: sanaa za maonyesho, ushairi, nathari n.k.
Ina tanzu tatu tu: ushairi, tamthilia na  riwaya
d)
Uwasilishaji: Huwasilishwa kwa njia ya simulizi ya mdomo. Hutegemea sauti
Huwasilishwa kwa njia ya maandishi.
e)
Mabadiliko: Hubadilika kulingana na mfumo wa kihistoria.  Aidha, fanani anaposimulia hadithi anaweza kuongeza au kupunguza jambo kila pale anapowasilisha sanaa yake. Pia, fanani akifa na kazi nayo italazimika kubadilika kutokana na yule atakayechukua nafasi yake.
Haibadiliki baada ya kuandikwa.
(f)
Wahusika: Wahusika wana uwezo wa kuchukua majukumu mawili kwa wakati mmoja. Mfano mhusika mtu anaweza kuwa pia mnyama. Wahusika wafuatao wanatambulika. (i) Msimuliaji (ii) Wasikilizaji
(iii) Wanyama (iv) Vitu na Mahali.

Kwa kawaida wahusika hushika jukumu moja kwa wakati mmoja. Wahusika wanaweza kuwa watu au wanyama au hata vitu, kama vile mti, jiwe, mwezi, nk..
(g)
Umiliki: Jamii nzima ndiyo inayohusika.
Umiliki: Mtunzi wa kazi hiyo ndiye anayehusika.


jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu 



Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

7 comments: