Njia zinazojitokeza katika uundaji wa msamiati ni
kama ifuatavyo:
Njia ya kutumia
mpangilio tofauti wa fonimu au vitamkwa: Kila lugha ina fonimu au sauti za
msingi ambazo hutumika kujenga silabi ambazo nazo hujenga maneno yote ya lugha
husika. Maneno mengi katika lugha huweza kupatikana kwa kubadili mpangilio wa
vitamkwa/sauti-fonimu za lugha husika.
Kwa mfano:
Sauti-fonimu /a/,
/o/, /n/ zikibadilishiwa mpangilio kwa namna mbalimbali zinaweza kuzalisha
maneno kama vile:
(i) o-n-a => ona (ii) => noa (iii) => oana.
Njia ya miambatano
yaani kuunganisha maneno: Hapa maneno mawili yanaunganishwa na kuwa neno moja. Kuna aina mbalimbali za miambatano:
(i) Miambatano kati ya jina huru na jina
huru.
mwana hewa
mwanahewa
mwana + nchi mwananchi
Afisa + misitu Afisamisitu
(ii) Miambatano kati ya Nomino na Kivumishi.
Mla + mbivu Mlambivu
Mwana
+ kwetu Mwanakwetu.
(iii) Miambatano
kati ya jina tegemezi na jina huru. Jina tegemezi linatokana na kitenzi.
Mpiga + maji
Mpigamaji.
Mpiga
+ mbizi Mpigambizi
(iv) Miambatano kati ya kitenzi na jina.
Piga + mbizi
pigambizi
Pima + maji
pimamaji
Kutohoa maneno:
Kila lugha ina uwezo wa kuchukua maneno kutoka kwenye lugha nyingine ili kukidhi haja ya mawasiliano kulingana na maendeleo ya jamii. Kiswahili nacho kimechukua maneno kutoka lugha mbalimbali za kigeni na lugha za Kibantu na kuyatohoa ili kusadifu misingi ya sarufi yake.
Kila lugha ina uwezo wa kuchukua maneno kutoka kwenye lugha nyingine ili kukidhi haja ya mawasiliano kulingana na maendeleo ya jamii. Kiswahili nacho kimechukua maneno kutoka lugha mbalimbali za kigeni na lugha za Kibantu na kuyatohoa ili kusadifu misingi ya sarufi yake.
Mfano:
(a) Kiingereza:
(i)
tractro => trekta => trekita =>
terekita
(ii)
plaugh => plau => pulau
(iii)
shirt => sheti => shati
(iv)
geography =>jiografia => jografia
(v) machine => mashine
(b) Kiarabu:
(i) laki => pokea
(ii)
ahadi => milele
(iii) dhaifu => nyonge
(iv)
ila => isipokuwa
(c) Kireno:
(i) bibo
=> bibo
(ii) roda => roda
(ii) mesa => meza
(iii) copa
=> kopa
(d) Kiajemi:
(i) bandar
=> bandari
(ii) dirisha => dirisha
(iii) kod => kodi
(iv) pilao
=> pilau.
(e) Kihindi:
(i) achari
=> achari
(ii) biyme
=> bima
(iii) ghati
=> gati
(iv) lakh
=> laki
(f) Kijerumani:
(i) schule
=> shule
(ii) hella
=> hela
(g) Kutoka
Lugha za Kibantu
(i) faculty
=> kitivo <kipare/kisambaa.
(ii) composite
=> kivung <kipare
(iii) state
house => ikulu <kigogo/kisukuma
(iv) national
assembly => bunge<kigogo/kisambaa
(v) fluid => ugiligili <kinyakyusa
Njia ya
urudufishaji:
Hii ni njia ya kurudia neno, likawa neon moja.
Hii ni njia ya kurudia neno, likawa neon moja.
Mfano:
(i) kimbele
=> kimbele mbele
(ii) pole => pole pole
(iii) kinyume => kinyume nyume
(iv) kimya => kimya kimya
(v) kizungu => kizungu zungu
Kwa
njia ya kufupisha maneno: Njia ya
kufupisha maneno inachukua ama herufu ama silabi ya kwanza ya kila neno
lililojitokeza katika jina zima la mahali au kitu funi.
Mfano:
(i) Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili => TUKI
(ii) Baraza la Kiswahili Tanzania => BAKITA
(iii) Chama Cha Mapinduzi => C.C.M
(iv) Baraza la Mitihani la Taifa => BAMITA
nk.
Njia ya kutumia mnyambuliko na uambishaji:
Neno jipya huundwa kwa kuunganisha viambishi kwenye mzizi au shina la neno. Njia hii hukuza lugha bila taabu kwani maneno ya lugha nyingi yanaweza kunyumbuliwa na kuambishwa, kama ifuatavyo:
(a) Mnyambuliko wa Majina:
(i)
taifa
=> taifisha => taifishwa => taifishiwa. nk.
(ii)
soma
=> somea => somesha => someshea => someshwa => someshewa =>
somesheka => , nk.
(b) Mnyambuliko wa Vitenzi:
(i) piga
=> pigana => pigisha =>
pigishwa => pigishia => pigia => pigiana, pigika, nk.
(ii) cheza
=> chezana => chezesha => chezeshwa => chezeshea => chezeana
=> chezwa => chezeka, nk.
(c) Mnyambuliko
wa Vivumishi:
(i)
fupi
=> fupisha => fupishia => fupishwa => fupishiwa => =>
fupishana => fupishika, nk.
(ii)
safi
=> safisha => safishana => safishia => safishiana => safishika,
nk.
(d) Mnyambuliko wa Vielezi:
(i) haraka
=> harakisha => harakishana => harakishika => harakishia =>
harakishiana, nk.
Njia ya Kutumia
Uambishaji
(i) taifa => utaifa, mataifa, utaifishaji, nk.
(ii) piga => kupigana, anapiga, nk.
(iii) safi => msafi, wasafi, nk.
(iv) haraka => kuharakisha, nk.
Njia ya kufananisha
sauti/umbo: Baadhi ya maneno ya
Kiswahili yametokana na mwigo wa sauti au dhana ya kitu fulani.
Mfano:
(i) Piki-piki-
piki-piki => pikipiki,
Neno
ambalo limetokana na mwigo wa sauti (mlio) wa chombo husika.
(ii) tu-tu-tu
=> mtutu (wa bunduki)
neno ambalo limetokana na mwigo wa sauti ya risasi inapotoka kwenye
bunduki baada ya kufyatuliwa.
(iii) kifaru
Hii ni zana ya kivita ambayo imepewa jina hilo kutokana na umbo lake lililofanana na mnyama
aitwaye kifaru.
Njia ya vijenzi/viundaji:
Mara nyingi vijenzi huunda neno ambalo huwa nomino. Vijenzi hupachikwa mwishoni mwa kitenzi ili kiwe nomino. Maneno yanayojitokeza huwa na maana na ngeli tafauti tafauti.
Vijenzi vitumikavyo
ni kama ifuatavyo:
Kijenzi Kitenzi Nomino
{i} jenga mjenzi
linda mlinzi
soma msomi
panda mpanzi
{ji} winda mwindaji
soma msomaji
sema msemaji
cheza mchezaji
linda mlindaji
{o} soma somo/masomo
sema msemo/misemo
cheza mchezo
{u} kua ukuu
tulia utulivu /mtulivu
tukuka utukufu/mtukufu
choka uchovu
{e} teua mteule
tuma mtume
kata mkate
umba kiumbe
jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu
MAREJELEO
Maganga (1997), OSW 102: Historia ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria
cha Tanzania.
Masebo, J. A. Nyengwine, N.
(2002), Nadharia ya Lugha ya Kiswahili,
Kidato cha 5 na 6. Aroplus
Industries Ltd: Dar es Salaam.
Nkwera, Fr. F. V. (2003), Sarufi, Fasihi na Uandishi wa Vitabu,
Sekondari na Vyuo. Creative Prints Ltd: Dar es Salaam.
Top 10 Best NetEnt Casinos in 2021 - CasinoWow
ReplyDeleteTop 10 NetEnt Casino Sites · 1. Red Tiger 메리트 카지노 도메인 – Best for Mobile Games · 2. LeoVegas – Best for Casino 퍼스트 카지노 Bonuses w88 · 더킹카지노 3. El Royale – Best for Live 메리트 카지노 조작 Casino Games.