MISINGI YA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI.
Uhakiki ni uchunguzi au uchambuzi wa kina wa kazi za fasihi. Uhakiki wa kazi yoyote ya fasihi unazingatia maeneo makuu mawili. Na Kazi za fasihi huhakikiwa kwa kutumia vigezo vikuu viwili maeneo hayo ni :
·
MAUDHUI.
·
FANI.
MAUDHUI.
Ni yale mambo yote ambayo yamemsukuma mwandishi /msanii
kuandika kazi yake.Na pia Maudhui ni
mambo anayoyasema msanii kwa walengwa au hadhira yake. Katika kipengele cha
maudhui mhakiki hana budi kuchambua mambo yafuatayo:
1.
DHAMIRA
2.
MIGOGORO.
3.
UJUMBE.
4.
FALSAFA.
5.
MTAZAMO.
6.
MSIMAMO.
DHAMIRA.
Ni suala linaloongelewa au
kujadiliwa na mwandishi au msanii katika kazi ya sanaa. Ni kiini cha habari
nzima iliyoandikwa au kusimuliwa.Ni wazo kuu au mawazo yanayojitokeza katika
kazi ya fasihi. Kwa mfano Ukombozi wa mwanamke,Rushwa na Umuhimu wa elimu.
MIGOGORO.
Ni mivutano au mikinzamo
inayojitokeza kutokana na misuguano ya kiuchumi,kisiasa kijamii na kiutamaduni
. Ni hali ya kutoelewana baina ya pande mbili. Migogoro yaweza kuwa baina ya
pande mbili au mtu binafsi. Kuna aina mbalimbali za migogoro. Aina hizo ni
pamoja na :
Kisiasa, kiuchumi,kijamii na
kinafsi.
UJUMBE.
Ni mafunzo au maadili
yanayopatikana baada ya kusoma kazi ya fasihi ili kuweza kupata ujumbe. Ujumbe unaweza kutamka wazi au kwa kificho. Mhakiki
hana budi kujiuliza maswali yafuatayo: mwandishi anatoa ujumbe gani kwa
jamii?,anashauri nini?,je ujumbe huo unamhusu nani katika jamii?
FALSAFA.
Ni mwelekeo wa imani ya msanii
,mwandishi au msanii anaamini nini Mfano unaweza kubaini imani ya mwandishi
Fulani kuhusu mwanamke au suala zima la maisha. Na pia unaweza kuijua vizuri
falsafa ya mwaandishi kwa kusoma kazi zaidi ya moja za mwandishi anayehusika.
MTAZAMO.
Ni namna mwandishi anavyoona mambo
, hapa mhakiki hana budi kubaini uyakinifu wa msanii. Mhakiki ajiulize je
msanii ameandika mambo kwa kubuni au kudhani au kiuyakinifu au ameichunguza
jamii kwa undani. Kwa mfano mtazamo wa kidini unaweza kumwongoza kuona kuwa,
kila jambo nimapenzi ya mungu.
MSIMAMO.
Ni uamuzi wa kufuata jambo Fulani
bila kujali kukubalika au kutokukubalika
kwa jambo hilo na jamii. Au ni maoni yake juu ya mambo mbalimbali
anayoyaeleza kwenye kazi yake.
FANI.
Kipengele cha fani hujumuisha mambo yafuatayo:
1.
MUUNDO.
2.
MTINDO.
3.
WAHUSIKA.
4.
MANDHARI.
5.
LUGHA.
MUUNDO.
Ni mtiririko au mpangilio wa
visa/matukio ya kazi ya fasihi. Katika kuhakiki muundo msanii anapaswa
kuchunguza kwa makini jinsi kazi ya fashii ilivyoundwa , namna tukio moja
lilivyounganishwa na jingine,kisa kimoja kinavyounganishwa kisa kingine.Mhakiki
achunguze mgawanyo wa sura katika riwaya.
AINA ZA MIUNDO.
Kuna aina kuu tatu za miundo
ambazo msanii anaweza kutumia katika kuwasilisha kazi yake:
1.
Muundo wa moja kwa moja (MSAGO).
2.
Muundo rejeshi.
3.
Muundo rukia.
MUUNDO WA MOJA KWA MOJA.
Ni mfuatano wa matukio toka tukio
la kwanza hadi mwisho huwa ni wa moja. Mhusika huanza kusimuliwa toka
anazaliwa,anakua na hadi anakufa.
MUUNDO REJESHI.
Ni muundo wa kiuchangamano zaidi
ambao hutumia urejeshi amakwa kumpeleka msomaji mbele au kumrudisha nyuma
katika mpangilio wa matukio.
MUUNDO RUKIA.
Ni muudo ambao visa husimuliwa kwa
kurukiana, muundo huu huwa na visa viwili ambavyo husimuliwa kwa kurukiana, mwishoni visa hivyo huungana
na kujenga kisa kimoja.
MTINDO.
Ni namna msanii anavyowasilisha
kazi yake. Mtindo ni sifa mojawapo pambanua ambayo humtofautishaa msanii mmoja
na mwingine. Aidha katika kipengele hiki cha mtindo mhakiki hulazimika
kuchunguza yafuataayo: matumizi ya nafsi, matumizi ya masimulizi,monolojia au
dialojiaa, matumizi ya barua, matumizi ya lugha nyingine nje ya kiswahili kama
kiingereza.
WAHUSIKA.
Ni watu au viumbe vinavyowakilisha
watu katika kazi za fashi. Uwakilishi huo huhusu hali halisi ya maisha jamii
inayohusika. Aidha wahusika hubeba mawazo ya msanii na kubeba migogoro ya
kijamii inayozungumziwa katika kazi ya
fasihi.
AINA ZA WAHUSIKA.
Kuna aina mbili za wahusika:
1.
Wahusika wakuu.
Ni mhusika wa muhimu kuliko wote. Huyu huonekana kuanzia
mwanzo hadi mwisho wa kazi ya fashi.
Huyu ndiye hubeba dhamira au mawazo makuu ya msanii.
2.
Wahusika wadogo.
Ni wahusika ambao wanaoonekana
mara chache na kazi yao nikusaidia kumdhihirisha zaidi mhusika mkuu.
MANDHARI.
Ni sehemu ambapo au mazingira
ambako matukio ya hadithi au masimulizi yanafaanyika .kazi fasihi hujengwa
katika mazingira maalum ambayo huitwa mandhari. Mandhari katika kazi ya fashi
husaidia kuleta hisia iliyokusudiwa. Mfano kama msanii anakusudia kuleta hisia
ya woga humlazimu kuchukua mandhari ya woga kama msitu mnene, ngurumo za
wanyama wakali.
LUGHA.
Ni kiungo muhimu sana katika kazi
yoyote ile ya fasihi japokuwa lugha inayotumika katika kazi ya fasihi haina
budi kuwa ni ya kisanaa zaidi ili kuweza kuibua hisia kwa hadhira yake.Ni lugha
ambayo huwa na mvuto wa moja kwa moja kwa wasomaji wake kutokana na vionjo
mbalimbali ambavyo msanii huvichanganya katika kumvuta msomaji kwa kuzingatia
matumizi ya lugha fasaha, utenzi wa misamiati , matumizi ya misemo na tamathali
za semi huongeza utamu na kufanya kuwa hai.
TAMATHALI ZA SEMI.
Ni semi ambazo hupamba lugha kwa
kiasi kikubwa.Baadhi ya tamathalihizo ni pamojana
1.
SITIARI.
Ni semi inayolinganisha matendo vitu au tabia
tofauti bila kiunganisha.
Mfano
Neema ni malaika.
2.
TASHBIHA.
Ni semi zinazounganisha vitu kwa kutumia
viunganishi kama NI,MITHILI,WA ,KAMA N.K
kwa mfano Ana wembamba kama
mlingoti.
3.
TASHIHISI.
Ni semi ambazo vitu visivyokuwa watu hupewa sifa
hizo.
Mfano
Miti ililalamika siku kucha kwa
upepo mkali.
4.
MUBALAGHA.
Ni semi ambazo hukuza sana jambo
kupita kiasi.
Mfano Sauti yake inaweza kumtoa nyoka pangoni.
Mfano alimlilia mumewe hadi
kukawa na bahari ya machozi.
5.
DHIHAKA.
Ni semi ambazo hutumia mafumbo.
6.
TAFSIDA.
Ni semi ambazo hupunguza ukali wa
maneno.
Mfano Amejifungua badala ya
amezaa.
7.
KEJELI.
Ni semi ambazo hutumia lugha ya
kejeli katika kutoa ujumbe.
8.
TAKRIRI.
Ni semi ambazo baadhi ya maneno
fulani hurudiwarudiwa kwa lengo la kuonesha msisitizo.
Mfano kutwa,kucha,kutwa,kucha jambo ni
hilohilo tu!
9.
MJALIZO.
Ni semi ambazo huorodhesha vitu bila kutumia
alama za mkato.
jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu
0 comments:
Post a Comment