NGELI ZA NOMINO:


NGELI ZA NOMINO:

Ni utaratibu unaotumika kuweka nomino katika mpangilio au kupanga nomino katika makundi yenye  nomino zinazofanana. Mfano maneno mtoto na mjomba yako katika ngeli moja, kwa sababu katika umoja, yote yanaanza na m huku vitenzi vyake vikianza na a.

AINA ZA NGELI ZA NOMINO:
Kwakuzingatia kigezo cha upatanisho wa kisarufi, kuna ngeli tisa za nomino.ngeli hizoni:
1.   
          NGELI YA   a-wa :
Ngeli hii inajumuisha majina ya viumbe hai,kama vile watu, wadudu.
Kwa mfano:
Njiwa anapaa.  – Njiwa wanapaa.
2. 
           NGELI YA  u-ya:
Ngeli hii inajumuisha nomino ambazo zina kiambishi awali  u- katika umoja na ma- katika wingi.
Mfano:
Uuaji umedhibitiwa – Mauaji yamedhibitiwa.
3.
           NGELI YA u-zi.
Ngeli hii inajumuisha majina yenye viambishi awali u- na w- katika umoja zi- katika katika wingi:
Mfano:
Wembe umevunjika  - Nyembe zimevunjika.
4
  .       NGELI YA u-i:
Ngeli hii inajumuisha majina ya baadhi ya sehemu za mwili,kama vile mikono, miguun.k.
Mfano:
Mguu umepinda.- Miguu imepinda.
5
 .       NGELI YA li-ya:
Ngeli hii inajumuisha majina ambayo yana kiambishi awali li- katika umoja na ya- katika wingi:
Mfano:
Gari limeanguka  -  Magari yameanguka.
6.   
         NGELI YA ki-vi:
Ngeli hii inajumuisha  majina ya vitu visivyo hai.kama vile kisima, kitanda.
Mfano:
Chuma kimepinda. – Vyuma vimepinda.
7.
       NGELI YA  ku-:
Ngeli hii inajumuisha majina yote yanayotokana na kunominishwa kwa vitenzi. Kama vile kusoma.
kwa mfano:
Kulala  kunasaidia.
8.
        NGELI YA  i-zi:
Ngeli hii inajumuisha majina ambayo ayabadiliki umbo katika umoja na katika wingi.
Mfano:
Njia ina majani. – Njia zina majani.
9.     
          NGELI YA  pa/mu/ku:
Ngeli hii inajumuisha majina yanayoonesha mahali.
Mfano:
Mahali  pale  palitumikaa.
Mahali  mule  mulikodiwa.
Mahali  kule  kunauzwa


Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment