ni sehemu ya neno inayobakia mara baada ya kuondoa viambishi vyote vya awali na tamati katika neno hilo.
Mfano: - a-na-chez-a {-chez-}, m-ku-lim-a {-lim-}
Aina za mzizi.
Mzizi funge ni ule ambao hauwezi kujikamilisha kimaana yaani hauwezi kusimama kama neno.
Mfano; -lim-, -chez-, -imb- n.k.
Mzizi huru ni ule ambao huweza kusimama kama neno na ukichanganuliwa zaidi hupoteza maana yake ya msingi.
Mfano; Kinu, Kazi, Arifu, Sali n.k.
Shina la kitenzi
ni sehemu ya neno ambayo huongezwa viambishi fuatishi (tamati) au ni sehemu ya neno ambayo hubakia baada ya kuondolewa viambishi tangulizi.
Mfano:- chez+a = cheza, lim+a = lima. Sehemu hii ya neno hutumika kuundia neno jipya.
Aina za shina.
Shina sahili – hili ni shina ambalo huundwa na mofimu moja tu ambayo ni mzizi wa neno hilo, huwa ni mofimu huru,
Mfano; Kesho, jana, kitabu, jarida n.k.
Shina changamano – shina hili huundwa na mzizi na kiambishi tamati maana.
Mfano; cheka, lala, lia, kula n.k
Shina ambatani – shina hili huundwa na mofimu mbili ambazo ni huru.
Mfano; mwana + kwenda = mwanakwenda, mbwa + mwitu = mbwamwitu
0 comments:
Post a Comment