Tabia ya Lugha
Zifuatazo ndizo tabia zinazojitokeza kwa kila lugha; tabia ambazo
zinaihalalisha lugha yo yote kuwa lugha na si vinginevyo.
(i) Lugha Ina Tabia ya Kukua
Lugha hukua kadri inavyoendelea kutumiwa na jamii. Maneno ya zamani yanabadilika, yote haya ni kutokana na mahitaji ya umma au jamii katika harakati za wana-jamii wake kujiboresha kimaendeleo ambako wakati mwingine si rahisi kutokana na misukosuko duniani. Kwa hiyo, kama lugha itakosa watumiaji.
(ii) Lugha Ina Tabia ya
Kuathiriwa
Lugha inaweza kuathiriwa na lugha nyingine au inaweza kuathiri lugha
nyingine. Mfano lugha ya Kiswahili imeathiriwa sana na lugha ya Kiarabu,
Kibantu na Kiingereza. Vile vile Kiswahili kimeathiri lugha hizo.
(iii) Hakuna Lugha Bora
Lugha zote ni bora. Ubora wa lugha upo kwa wale
wanaotumia. Lakini pia kuna lugha bora na
bora lugha. Bora lugha hujitokeza kwenye misimbo na/au rejesta.
(iv) Kujitosheleza
Kila lugha inajitosheleza kulingana na mahitaji ya
jamii ambayo inatumia lugha yenyewe katika kipindi husika cha maisha yake hiyo
jamii.
Sifa za Lugha
Zifuatazo ndizo sifa zinazojitokeza kwa kila lugha; sifa ambazo
zinaihalalisha lugha yo yote kuwa lugha na si vinginevyo.
(i) Lugha ni Lazima Imuhusu
Mwanadamu
Kimsingi hakuna kiumbe kisicho mwanadamu (mtu) kinachoweza kuzungumza
lugha. Lugha ni chombo maalum wanachokitumia binadamu kwa lengo la mawasiliano.
(ii) Sauti
Lugha huambatana na sauti za binadamu kutoka kinywani mwake binadamu
lazima atamke jambo kwa sauti.
(iii) Lugha Huzingatia
Utaratibu Maalum
Lugha
ni Sauti Zenye Utaratibu Maalumu
Sauti za lugha yoyote huwa zimepangwa kwa kufuata
utaratibu fulani unaokubaliwa na jamii hiyo ya watu. Kwa maneno mengine si kila
sauti itokayo kinywani mwa mwanadamu ni lugha. Mtoto anapolia hatusemi anaongea
au anazungumza. Utaratibu huo huitwa sarufi.
Mfano:
(a) Hatusemi
(i) John embe ana [joniembeana] au [joninaembea].
(ii) Kisu changu
mimi nimepoteza
[kisuchangumiminimepoteza]
(b) Jamii
imepatana kusema
(i) John ana embe [jonianaembe]
(ii) Mimi nimepoteza kisu changu
[miminimepotezakisuchangu]
(iv) Lugha Hufuata Misingi ya
Fonimu
Lugha ina vitamkwa/vipashio
ambavyo huitwa fonimu. Wana-Isimu
wanakubaliana kwa ujumla kwamba fonimu ni
sauti yenye uwezo wa kuleta tofauti katika maana ikipachikwa katika neno la
lugha husika. Fonimu itazungumziwa kwa kirefu katika Mhadhara wa Tatu.
Kwa mfano, baadhi ya fonimu za Kiswahili ni:
·
/a/, /e/,
/i/, /o/, /u/,
Katika: [tata] ~ [teta] ~ [tita] ~ [tota]
~ [tuta].
·
/p/, /b/,
/t/, /d/, /c/, / ɟ /, /k/, /g/, /s/, /z/, nk.
Katika:
pawa~bawa~tawa~dawa~chawa~jawa
kawa~gawa~sawa~zawa, nk.
(v) Lugha Hufuata Mpangilio
wa Vipashio Unaoleta Maana
Muundo wa Lugha inayohusika kwa
mujibu wa mpangilio wa vipashio vyake lazima ufahamike. Mpangilio huo huanza na
fonimu, neno, kirai, kishazi, sentensi.
(vi) Lugha Inajizalisha
Vipashio vinavyoiunda lugha husika huwa na sifa ya kuweza kunyumbulishwa
ili kupata maneno mapya. Kwa mfano, vitenzi hunyumbulishwa kwa
kuongezewa viambishi na kwa hiyo, lugha hujiongezea maneno mapya. Ona:
(i) chez-a => ku-chez-a => ku-m-chez-a >
tu-li-m-chez-a.
(ii) chez-e-a =>chez-esh—a => chez-esh-an-a =>
chez-esh-an-ik-a.
(iii) chez-e-a =>chez-ek-a.
(vii) Lugha
Husharabu
Lugha husharabu kwa maana ya
kwamba lugha huchukua maneno kutoka lugha nyingine ili kujiongezea msamiati
wake. Tabia hii inazisaidia sana
lugha zinazokua.
kazi nzuri wa ustadi kuntu sufufu
ReplyDelete