(i) Rejesta
za Mitaani
Haya ni mazungumzo
yanayozungumzwa magengeni nayo hueleweka na wazungumzaji wenyewe. Ni lugha
ambayo huchipuka kutokana na kikundi cha watu ambacho ni kidogo. Lugha hii
hudumu kwa muda mfupi tu, halafu hufifia. Wakati mwingine lugha hiyo hukubaliwa
na jamii na kuweza kuingizwa katika msamiati wa lugha hiyo. Mfano wa maneno
yanayotumika sana mitaani ni kama vile “Mshikaji” (rafiki) Demu” (mwanamke),
“Nina waya” (sina pesa), “Kumwaga unga” (kupoteza kazi), umenoa” (umekosa),
(mambo safi), n.k. Kwa ujumla lugha
ya mitaani ni lugha isiyo sanifu, ni lugha iliyojaa maneno ya mitaani ambayo
yanaeleweka wa wazungumzaji wenyewe.
Mfano:
Ee bwana we! Maana hiyo Benzi
ilikuja kitututu-wangu wangu! Bila kutazama mbele kunakuja nini, basi akamwingia
babu wa watu-akamrusha kama
mpira, alipofika chini, kwisha habari
yake! Kichwa kama chapati. Simbaa wa mji watatumaliza...
(ii) Mazungumzo ya Kwenye Shughuli Maalum (Rejesta za Mahali)
Mazungumzo ya kwenye shughuli
maalumu hayafanywi kiholela, bali yanafuata taratibu na kanuni maalum
zinazojitokeza katika mazingira haya. Kutokana na kutumiwa kwake kwa muda mrefu
kwenye mazingira yale yale.
Mazungumzo ya kwenye shughuli
maalumu ni kama vile mazungumzo ya:
-
Maofisini
au mahali popote pa kazi
-
Mahakamani
-
Hotelini
-
Hospitalini
-
Msikitini
-
Kanisani n.k
(a)
Mazungumzo
ya mahotelini yana utaratibu wake ambao katika hali ya kawaida inaweza
isieleweke.
Mfano:
A: Nani wali kuku
B: Mimi
A: Chai moja wapi?
B: Hapa
Katika mazungumzo haya A
anapouliza “Nani wali kuku”: ana maana kuwa nani anahitaji kula wali na nyama
ya kuku”. Hapa hana maana ya kumwainisha mtu aitwaaye “wali kuku”.
(b)
Kwa
upande wa lugha ya mahakamani ni tofauti a lugha ya hotelini. Lugha ya
mahakamani inasisitiza usahihi ili
kuondoa migongano miongoni mwa wanaohusika.
Mfano:
Wakili wa Utetezi: Nakuuliza jaribio la kutaka kupindua serikali litakuwa kosa la
namna gani katika sheria za Kenya?
Kamishna Msaidizi: (Baada ya kupewa kitabu cha sheria za Kenya na kukisoma) Ni kosa la
uhaini.
Wakili wa Utetezi: Ulichukua muda mrefu kufikia jibu hili. Washitakiwa wawili
hawahusiani na makosa haya?
Kamishna Msaidizi: Sijui. (Uhuru, 26 Agosti, 1982:4).
Kimsingi hii ni hali ya kawaida
kabisa katika mahojiano ya mahakamani. Mara nyingi mahojiano katika mahakama
hayaendi haraka sana. Kila mtu anayehusika – hakimu, mwendesha mashtaka,
wakili, mdaiwa, shahidi, n.k. hujieleza kwa wazi wazi bila kujali urefu wa
maelezo.
(iii) Rejesta Zinazohusu Watu
Rejesta zinazohusu watu ni yale
mawasiliano yasiyo rasmi ni yale maongezi ya kawaida ya kila siku au mazungumzo
rasmi; kwa mfano mazungumzo kati ya:
-
Vijana
wenye rika moja,
-
Wazee
wenyewe,
-
Wanawake
wenyewe,
-
Wanaume
wenyewe,
-
Mwalimu
na mwanafunzi,
-
Meneja na
wafanyakazi wake,
-
Mtu na
mpenzi wake, n.k.
(c)
Mazungumzo
miongoni mwa marafiki wa rika moja huzungumza lugha ambayo wao wenyewe
wanaielewa na sio rahisi kwa mtu wa rika lingine kuielewa lugha hiyo.
Mfano:
‘Basi, Master jana wikiendi ilikuwa kibaridi sana’
‘Basi nilizamia infoo kwenye
zinga la mnuso huko saiti za upanga’
‘Nilifika getini nikakuta baunsa
kanyuti chedro likisubiri kumtoa
noma kila mzamiaji’
Alikuwa mnoko kishenzi’
‘Akatema mkwala mbuzi, nikajibu
kwa mkwala dume....
akabloo mimi ndani’.
Maana ya Maneno
Wikiendi – Mwisho wa wiki.
Kibaridi –tulivu.
Kuzamia infoo – Kuingia mahali
bila kualikwa.
Zinga la Mnuso –sherehe kubwa.
Saiti –sehemu.
Baunsa limenyuti chedro – Ni
mlinzi wa mlangoni ametulia pembeni.
Noma – Hatari.
Mnoko kishenzi – kinaa sana
Mkwala mbuzi – Vitisho dhaifu (Sani,
Toleo Na 49).
Mtu asomapo maelezo hayo, mara
moja unaona jinsi vijana hawa wa rika moja waishio mjini wanavyozungumza
Kiswahili. Si rahisi kwa mzungumzaji wa Kiswahili sanifu kuielewa kirahisi
lugha hiyo.
Mfano mwingine wa wazungumzaji
wa Kiswahili wa rika moja. Mzungumzaji Mkuu ni Chek Bob.
Yee! Mjumbe, degree kama degree
mimi oyee tu. Nadhania umeiget fresh kuhusu nguvu-nguvu kazi au vipi?. Mimi ndo
longtime niko hapa town bila Job nadunda na mensheni tu. Na vile vile ndo nina
wiki ee tu tangu niopoe hiki kikwapa. Wewe mwenyewe ukikicheki kikwapa chenyewe
waa! Sasa kwende nacho bush nishai au vipi mjumbe? Serikali yeneywe inatutia
mikwala sana. Sasa shika hivi visimbi vya anda bee na kitembo (210) kusudi mimi
nibane hapa hapa town. Hawa kinaa watilie mikwala mingi kwamba mimi ndo
longtime nina Job. Kwani misheni hii ikijipa utaipata wewe mwenyewe mjumbe!.
(Mfanyakazi Machi, 1988). Huu ni mfano mwingine wa kijana wa mjini, lakini
anamweleza mjumbe hisia na maoni yake.
(iv) Lugha
ya Kitarafa
Hiki ni Kiswahili cha tarafa
fulani. Ukikisema katika tarafa nyingine huwa ni vigumu watu wa sehemu hiyo
kuelewa unasema nini. Kwa ujumla ni Kiswahili ambacho kimeathiriwa na vilugha,
yaani lugha-mama.
Kwa mfano:
Kiswahili cha Kiyao – John
amenitona (amenifinya).
Kiswahili cha Kingoni – Mtambo
mrefu (muda mrefu).
Kiswahili cha Kimakonde –
Achante chana (asante sana).
Kiswahili cha Kinyakyusa – Kyama
Kya Mapindusi (Chama cha Mapinduzi), n.k.
(v) Kiswahili Rasmi/Sanifu
Ni msawazisho kutokana na
vilugha vya lugha ya Kiswahili. Kiswahili hiki hukubaliwa na wengi katika nchi
na ndicho kitumikacho katika shughuli za
kiserikali, kisiasa, elimu, uchumi, na vyombo vya habari hutumia lugha
hii. Mtu akizungumza lugha rasmi ni vigumu kumtambua anatoka sehemu gani ya
nchi. Kiswahili rasmi nchini Tanzania kinatokana na lahaja ya Kiunguja.
jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu
jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu
Mbona notes zenu zimekatwa hazionekana zote kwa nini hapa rekebisheni mitambo
ReplyDeleteaina za maneno iko wapi
ReplyDeleteAngalia hapa
Deletehttps://www.google.com/url?sa=t&source=web&rct=j&opi=89978449&url=http://petermwiza.blogspot.com/2014/04/aina-za-sentesi.html%3Fm%3D1&ved=2ahUKEwi67K72x5WBAxUEQ_EDHYxrBRoQFnoECCQQAQ&usg=AOvVaw1YwQ8ICrkUqvmNY986ZYMX
Naipenda kiswahili
ReplyDeletemaswal[ ziko wapi
ReplyDelete