KUENEA KWA KISWAHILI NCHINI KENYA WAKATI WA UKOLONI




Maganga, (1997:iv) anatufahamisha kwamba maandishi ya Kiswahili yalianza kutumika mapema zaidi Kenya kuliko sehemu nyingine ya Afrika Mashariki. Tenzi nyingi za Kiswahili ziliandikwa katika Pwani ya ya Kenya kama vile Lamu, Malindi na Mombasa. Kwa ujumla matumizi ya lugha ya Kiswahili nchini Kenya yameanza karne zilizopita.
Lahaja zitumikazo nchini humo ni pamoja na Kimvita, Kijomvu, Kingare Kichifundi, Kivumba, Kiamu, Kibajuni, Kipate na Kisiu. Lahaja hizi za Kiswahili ni tawi la shina kubwa la lahaja za Kibantu zinazozungumzwa nchini Kenya.

1   Baadhi ya Sababu Zilizokwamisha Maendeleo ya Kiswahili Nchini Kenya
Nchini Kenya, pamoja na kwamba Kiswahili kilianza karne na karne, lakini maendeleo yake yalikuwa duni sana wakati wa ukoloni ukilinganisha na ilivyokuwa kwa Tanganyika. Baadhi ya sababu zilizokwamisha maendeleo ya Kiswahili nchini Kenya ni kama ifuatavyo:
 (a)   Nchini Kenya lugha ya Kiswahili haikutiliwa maanani sana katika kufundishia. Lugha za Kienyeji zilitumika kufundishia katika Shule za Msingi. Baadaye walitumia Kiingereza, Kiswahili kilifundishwa kama somo tu. Kutokana na hayo Kiswahili nchini Kenya hakikupamba moto kama ilivyokuwa Tanganyika.

(b)    Kiswahili kilienea sehemu za Pwani tu ya nchi ya Kenya, watu  wa Kenya Bara hawakuwa tayari kuipokea lugha hii ya Kiswahili kwa sababu hawakuipenda; aghalabu, waliihusisha na dini ya ki-Islamu, jambo ambalo hawakuwa tayari kulipokea. Leo sote tunafahamu kwamba uhusishwaji wa lugha ya Kiswahili na dini ya ki-Islamu ulikuwa wa kimakosa kwa sababu kadhaa tuzijuazo.

(c)    Lugha zao za makabila makubwa kama vile Kikuyu na Kikamba waliona watazishushia hadhi  wakiongea Kiswahili badala yake.

(d)    Wamishenari wa Kenya walipenda kufundishia kwa Lugha za Kienyeji. Kiswahili kilitumika iwapo ilikuwa lazima tu kwa kuelewana na Wageni ambao walikuwa hawajui kilugha au Kiingereza.

(e)    Kwa upande wa biashara, misafara yote ya kibiashara ambayo aghalabu ilianzia Pwani kuelekea Bara ilikwamishwa na makabila makali, kama vile Wamasai na Wakwavi. Makabila hayo yalizuia Wageni wasipite katika maeneo makubwa ya Kenya, na kwa hivyo,  kuyazuia maeneo hayo yasifikiwe na misafara ya wageni hao kwa muda mrefu. Tatizo jingine lililosababisha misafara kutoka pwani ishindwe kupenya bara la Kenya ni la wanyama wakali katika mbuga za Tsavo.

(f)       Kiswahili kilionekana kuwa lugha duni na kutopendwa na wengi.
Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

2 comments:

  1. Asante sana kwa taarifa hii.Swali langu ni je, tunaweza je kujaza nafasi au pengo lililoachwa na mambo hayo uliotupa ili kukuza na kuendeleza lugha ya kiswahili pamoja na kuilinda lugha ya Kiswahili?

    ReplyDelete
  2. Naomba maelezo kuhusu sentensi tegemezi.

    ReplyDelete