AINA ZA SENTENSI


       


1 Sentensi Shurutia.
ni sentensi inayohuundwa kwa viambishii kama -ngeli-, -nge-, na -ngali-.
kwa mfano:
(1) ningelikutana naye angelinisaidia sana.

vilevile  aina hii ya sentensi hutumia kiambishi -ki-;
kwa mfano:
(1) ni kimwona tu nitakwambia.
                       
2   Sentesi-Sahili
Sentesi sahili ni kifungu cha maneno chenye kiima na kiarifu na chenye kuleta maana kamili iliyokusudiwa. Isitoshe, hii ni sentesi ambayo haifungamani na sentesi nyingine yo yote. 

Mifano:
(i)        Huu si ugonjwa wa kutisha.
(ii)       Mama anapanda mahindi.
(iii)     Mbunge wetu anahutubia.

Katika sentesi-sahili  (i) – (iii), zote ni sentesi sahili ambazo kila moja ina kiima kimoja na kiarifu kimoja.Aidha, zote huleta maana kamili.

3   Sentesi Ambatani
Sentesi ambatani ni sentesi iliyoundwa ama kwa kuambatanisha au kuunganisha:
           
           
Mifano:
(a)       Sentesi-sahili  na Sentesi sahili;
(i)          Khamisi alifika na Asha akaimba sana.                  
(ii)       Mgonjwa hali wala haendi choo.
(iii)     Mama analima shambani lakini Baba yeye halimi.
(iv)     Yosefu anakunywa sana pombe ila sigara havuti.

au
                       
(b)       Sentesi sahili na Sentesi changamani;
(i)          Khamisi alifika ukumbini na Binti aliyemwimbia akachoka.     
(ii)       Mkewe hampelekei mumewe chakula sipitalini wala waliopenda hawamletei cho chote.
(iii)     Mama mdhaifu anafanya kazi kila siku lakini Baba aliye na afya nzuri hafanyi kazi.
(iv)     Watu wanene hawali sana ila wembamba hula sana.
           
au
 (c)      Sentesi-changamani na Sentesi-changamani;  
(i)     Khamisi alipofika ukumbini akaketi na binti aliyemwimbia akachoka baada ya saa moja. 
(ii)    Wasanii walipoingia ukumbini hawakuimba wala hawakucheza walipotakiwa kufanya hivyo.
(iii) Mama asipofanya kazi husemwa lakini baba asipofanya kazi hasemwi.
(iv)   Watu walio wembamba hula sana ila wasio wembamba hawali sana.
        


.4   Sentesi Changamani
Sentesi-changamani ni sentesi iliyoundwa kwa sentesi sahili na tungo tegemezi. Kwa kuwa maana ya tungo tegemezi hukamilishwa na maana ya sentesi sahili, sentesi changamani hujitokeza kama sentesi mchanganyiko, yaani maana za sentesi-mbili sahili zilizochanganyishwa.                                      
Mifano:
(i)        Binti ambaye hakufika jana, asimame.
(ii)       Viti ambavyo vimevunjika, tutavitengeneza.
(iii)     Wanaojidai shupavu, mkamfunge paka kengele). nk.


JOIN OUR WHATSAPP MATERIAL GROUP

BOFYA👉 PRIMARY MATERIAL GROUP 

BOFYA👉 SECONDARY MATERIAL GROUP

BOFYA👉 ADVANCE MATERIAL GROUP  

BOFYA👉 NURSERY MATERIAL GROUP



Jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu. 



MAREJELEO



Maganga (1997), OSW 102: Historia ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.
Masebo, J. A. Nyengwine, N. (2002), Nadharia ya Lugha ya Kiswahili, Kidato cha 5 na 6.  Aroplus Industries Ltd: Dar es Salaam.
Nkwera, Fr. F. V. (2003), Sarufi, Fasihi na Uandishi wa Vitabu, Sekondari na Vyuo. Creative Prints Ltd: Dar es Salaam.

Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

3 comments:

  1. Hivi tukisema " Sentensi shurutia" , hapo tunakuwa tumezingatia kigezo cha muundo au cha dhamira??

    Ninahitaji jibu

    ReplyDelete