(i) Kuburudisha
Fasihi simulizi huweza kutumiwa kama burudani kwenye mkusanyiko wa
jamii. Tanzu kama hadithi, ushairi, semi (methali, vitendawili, nk.) aghalabu
hutumiwa ili kuwaburudisha waliokusanyika katika jamii. Kwa mfano, watoto
wanapokusanyika kucheza, aghalabu hutegeana vitendawili kama njia ya
kujiburudisha. Hadithi, ngano, hekaya au hata hurafa huweza pia kutambwa kama
njia ya burudani.
(ii)
Kuelimisha
Kwa kutumia fasihi simulizi, wanajamii wanaweza kuzielimisha thamani za
kijamii, historia yao, utamaduni na mtazamo wao kilimwengu kutoka kizazi kimoja
hadi chengine.
(iii)
Kuipa
Jamii Muelekeo
Kwa njia ya kuelimishana kimawazo yanayohusiana na tamaduni na desturi
za jamii husika, wanajamii wanahakikisha kwamba jamii, kwa kutumia fasihi
simulizi, inapata muelekeo utakaowabainisha wao mbali na wengine.
(iv)
Kuhifadhi
Historia na Utamaduni
Katika kuhifadhi amali muhimu za
kijamii, fasihi simulizi inakuwa nyezo muhimu. Aidha, wanajamii
hufahamishwa kifasihi simulizi historia yao – wao ni nani na wanachimbukia
wapi. Maarifa haya ni muhimu kwa kila mwanajamii, kwani yanamsaidia sio tu
kujielewa, bali pia kujitambua.
(v) Kuunganisha
Vizazi vya Jamii
Fasihi simulizi ni msingi mkubwa wa kuwaunganisha wanajamii waliopo na
waliotangulia mbele ya haki. Kwa kutambiwa hadithi, vitendawili, methali na
nyimbo zao, umbali wa kiwakati kati ya vizazi vilivyotangulia mbele ya haki,
vilivyopo na vijavyo unafupishwa kwa kiasi kikubwa sana.
(vi)
Kufundisha
Jamii ina jukumu la kuwafundisha vijana wake maadili ya jamii ile
ambayo yana adili yaani funzo au ujumbe
unaowaelekeza, kuwaadibu, kuwaonya na kuwaongoza kwenye matarajio ya jamii ile.
Kwa hiyo, jamii nyingi hutumia fasihi simulizi kama njia ya kuwaelekeza na
kuwafundisha vijana wake mwenendo mzuri, maadili na falsafa ifaayo ili kutunza
jina na heshima ya jamii ile. Kwa mfano, katika vita dhidi ya Nduli Iddi Amini
1978/1979 nyimbo za kwaya, nyimbo za muziki wa dansi, tenzi, mashairi n.k.
zilitumika kuongeza hamasa kwa askari wetu waliokuwa mstari wa mbele vitani
kuwaongezea ari ya kumwadhibu adui yetu. Kitendo cha kushindwa kwa Iddi Amini
katika vita vile tunaweza kusema kwamba kazi hizo za fasihi simulizi zimefaulu
katika dhima yake ya kuelimisha ili kuongeza hamasa kwa askari wetu. Umuhimu wa
fasihi unaonekana katika kufaulu kutatua matatizo yetu katika jamii.
(vii)
Kuukuza
Ushirikiano
Ilivyo ni kwamba fasihi
simulizi ni mali ya jamii wala sio ya mtu binafsi. Hadithi inaposimuliwa kwa
hadhira kubwa, vitendawili vinapotegewa kundi pana, ni kwa sababu kimsingi
fasihi simulizi ndivyo ilivyokusudiwa itumike katika muktadha wa kuvihusisha
sio vikundi vidogo vidogo tu, bali pia, na hasa jamii nzima.kwa jumla.
(viii)
Kuzikuza
na Kuziendeleza Stadi za Lugha
Kwa kuwa fasihi simulizi hutegemea usemi
na matamko, hatuwezi kushiriki
katika kusimulia hadithi, kutegeana vitendawili, kuimba, nk. bila ya kuongea au
kutamka au kuimba. Kwa sababu hii, fasihi simulizi ina mchango mkubwa wa
kuboresha uwezo wetu wa kuzimiliki na kuzimudu stadi za lugha. Kwa mfano, tanzu
za vitanza ulimi zilisaidia kuhakikisha kwamba utamkaji ni mzuri; utegeanaji wa
vitendawili na majibu yake sahihi huukuza uwezo wa kuwaza haraka haraka na kwa
usahihi. Hadithi huukuza ule uwezo wa kukumbuka maudhui.
Hard working!
ReplyDeleteasante kaka karibu tena pia tunakaribisha maswali
ReplyDeleteasante kwa kazi nzuri
ReplyDeleteThis helped me a lot on my cambridge kiswahili subject cause i dont know kiswahili that much and we were given a swahili work about kazi za fasihi so this helped so much thank you mr Mwiza Peter so much
ReplyDeleteThis helped a lot cause i come from a cambridge school and they gave us a swahili project to do so this helped so much i do swahili dogo dogo
ReplyDeleteKaka kazi yako nzuri kabisa heko!
ReplyDeleteKaka kazi yako nzuri kabisa heko!
ReplyDeleteHongera sana Mwalimu kwa uthubutu wako hasa wa kutoa elimu kwa jamii. Huu ndio Uzalendo na Utaifa hasa ukiwa Mwalimu. Kutoa ni Moyo. Juhudi ya kuielimisha Jamii ni kielelezo tosha cha matumizi bora ya elimu uliyoipata. Endeleza kazi za kibunifu. Hii ndio hazina yako kuu.
ReplyDeleteNImependa sana kazi yako
ReplyDeleteAsante kwa kuwa nasi tunawapenda wote
ReplyDeleteKazi yako ni nzuri sanaaa
ReplyDeleteasanta mwalimu kwa kazi nzuri Mola akubariki
ReplyDeleteNahitaji umuhimu wa kufunza fasihi simulizi katika shule ya upili
ReplyDeleteHongera kwa KAZI ahali kama hii Jasusi awazidishie
ReplyDeleteniceeeeeee
ReplyDeleteCan't see on the side plz put all sides clear but gd work bro
ReplyDeleteNina swali
ReplyDeleteToa mifano ukieleza dhima ya fas oh I simulizi
Daaaa! Nimekipenda Sana hiui mtadao Asante Sana
ReplyDeleteImenisaidia kuweza kupata kazi ya ziada kila kitu . Asante sana mwiza Peter kwa kuleta hii mtandao.
ReplyDeletekazi safi kabisaa
ReplyDeleteAsante sanaa kwazi nzuri imenisaidia sana Mimi kama mwanafuzi
ReplyDeleteThanks 😊
ReplyDeleteAsante Sana umenisaidia, kazi ya,ziada 🙏
ReplyDelete