AINA ZA MANENO




                      Jina (J) au nomino

Kama vile: baba, mama, mwalimu, usingizi, fundi, njaa, Yusufu, Maria, nk. Majina ni mengi, lakini yote yamegawanywa katika makundi matatu:
                                               
(a)    Majina ya pekee, kama vile: Allah              
Yusufu, Maria, Iringa, nk.
         Majina ya pekee yanapoandikwa, aghalabu huanza na herufi kubwa.
                                               
(b)    Majina ya jumla: majina yote yasiyo ya pekee ambayo hutaja kitu kimoja au vitu vingi kwa pamoja, kama vile: mzazi, mwanamke, chakula, maji, hewa, nk.

(c)    Majina ya maarifa au Majina dhahania: ni majina ya vitu vya kufikirika, au hali, kama vile: uzuri, usingizi, uhodari, wekundu, woga, utamu, nk. Majina ya jumla na majina ya dhahania (maarifa) yanapoandikwa huanza kwa herufi ndogo, isipokuwa yakianza sentensi au yakiwa ni kichwa ha habari.

                                        

                                            Kivumishi (V)

Haya ni maneno au vifungu vya maneno vinavyopambanua au kueleza zaidi, yaani kuvumisha, habari kuhusu majina. Kuna aina nane (8) za vivumishi, navyo ni:

(a)       Vivumishi vya Sifa, kama vile: -ema, refu, kali, dogo, safi, chafu ,nk. katika: Mwalimu mwema, maji safi, kazi ndogo, nk.
                                               
(b)       Vivumishi vya Idadi, kama vile: moja, tatu, n’ne, tano, nane, sita, saba, tisa, kumi, nk. katika: Mwalimu mmoja,Walimu watatu, ..., Niuzie kuku sita, saba, tisa.
                                               
(c)       Vivumishi vya Kuonesha au Vivumishi Vioneshi, ni maneno yanayoonesha ujirani au umbali wa kitu au vitu. Mashina yake ni man’ne: hu-, hi-, ha-, kwa vitu vya karibu, na: -le, kwa vitu vya mbali na –lee, kwa watu au vitu vya mbali zaidi. Kwa mfano: mtu huyu, mtu yule, mtu yulee; watu hawa, watu wale, watu walee; vitu hivi, vitu vile, vitu vilee;...
                                               
(d)       Vivumishi vya Kuuliza au Vvivumishi Viulizi,vinaashiriwa na neno gani. Neno ‘gani’ linapotumika katika tungo, linahitaji ‘jibu ‘ linalotaja orodha au sifa ya hicho kitu ambacho habari zake zinaulizwa, kama vile: Mwanafunzi gani unamtaka? Jibu: mwema, hodari, wa darasa la tatu, nk.
                                               
(e)       Vivumishi vya Kumiliki au Vivumishi Vimilikishi, ni maneno yanayoonesha mtu au kitu/vitu ni ‘mali ya nani’. Kwa jumla, viko sita (6):
(i)                -angu ~ -etu (katika: mtoto wangu ~ mtoto wetu;         
(ii)             -ako ~ -enu; (katika: mtoto wako ~ mtoto wenu;                                   

(f)        Vivumishi vya A-unganishi, vimeundwa na vineno vidogo dogo ambavyo vinaishia na ‘a’.  Vineno hivi huunganisha majina mawili, vyenyewe vikiwa katikati, kama vile:
            (i)        mtu wa hekima;        (ii)       nyumba ya Baba;
            (iii)     kiti cha mbao;           (iv)      jino la tembo;
(v)       mahali pa Babu;       (vi)      Chumbani mwa Bibi; nk.                   

(g)       Vivumishi vya Majina au Vivumishi Majina, ni maneno ambayo yanaleta maana ya kivumishi, na kwa hiyo yanaweza kuvumisha majina mengine, kama vile:
 (i)       kipofu katika: Kijana kipofu;
(ii)       mtu shujaa husifiwa;
(iii)     bata mzinga;
(iv)      mwaka jana;
(v)       askari kanzu; nk..

(h)       Vivumishi vya –enye, -enyewe, -ote, -ingine, vina sifa ya kuvumisha majina au viwakilisha katika tungo, kama vile:
 (i)       -enye  huonesha kumiliki kitu fulani katika muundo wa A-unganishi, kama vile:
            Mtu mwenye busara  = mtu wa busara = mtu aliye        na busara.
(ii)       -enyewe huonesha na kurejesha nafsi.
           
    Mara nyingi, tendo la kuonesha na kurejesha nafsi hutokea pamoja kama vile: Mtu amejipiga mwenyewe’; Mtu mwenyewe amejipiga’;

   Mara nyengine husimama peke yake, kama vile: ‘Mwenyewe amekuja’.

            (iii)     -ote huonesha umoja usiogawika = kitu kamili kamili, kama vile:
.     Wali wote,               . Mboga yote.
.     Njia zote,     . Swali lote.
.     Mahali pote,  . Chumbani mwote, nk.
                                               
(iv)      -o –ote, huonesha kila kitu, kitu cho chote kiwacho kinahusika na jambo linalotajwa, kama vile: 
·        Kalia kiti cho chote.     
·        Nenda po pote lakini tunasema:         
·        Mtu, ng’ombe, kuku ye yote.
                                   
                      
                         
                                              Kiwakilishi (W)

Kiwakilishi ni neno mojawapo linaloweza kutumika badala ya jina (J). Kama vile:
  
(a)       Viwakilishi vya Kuonesha au Viwakilishi Vioneshi, kwa mfano:                                
(i)                Huyu ameleta asainimenti yake.
(ii)             Yule hajaileta.



Neno huyu, yule, hapa, kule yametumika badala ya majina; yamesimama badala ya majina; ni viwakilishi vya majina.   

(b)       Viwakilishi vya Kuuliza au Viwakilishi Viulizi huashiriwa na mofu {-pi}, ambayo katika tungo, hutanguliwa na kiambishi-ngeli cha jina husika, kama vile: 
(i)        Umesema ameleta asainimenti yake yupi?.
(ii)       Kauziwa shamba letu moja? Lipi?
(iii)     Ameenda wapi?
(iv)      Alikutuma nikupe ndizi ngapi?
lakini tunasema:
(i)        Wangapi wameleta asainimenti zao?
(ii)       Vingapi vimeharibika?  n.k

Aidha, maneno nani, nini na lini, kama vile:
(i)        Nani kaja?                
(ii)       Unakula nini?           Jibu   
(iii)     Mjomba kaja lini?   

(a)              Viwakilishi vya Kurejesha au Viwakilishi Virejeshi      
vimejengwa na shina {amba-} pamoja na vipande vidogo vidogo –ye, -o, -cho, -vyo, -lo, -po, -mo, -ko, nk., kama vile:
                                               
(i)          Mtu ambaye amekuja, namwomba tuonane.                                             
         Neno ambaye limetumika badala ya jina mtu.

(ii)       Neno ambalo umesema, halina mashiko.
Neno ambalo limetumika badala ya jina neno. 

(iii)     Mti ambao ameuangusha, umetufaa sana. Neno ambao limetumika badala ya jina mti. nk.

Elewa kwamba:
(i)        vipande vidogo vidogo –ye, -o, -cho, -vyo, -lo, -po, -mo, -ko, nk. vinachaguliwa kulingana na ngeli ya     majina yanayorejeshwa navyo.

(ii)       vipande vidogo vidogo hivyo au silabi –ye, -cho, -lo, -po, ... vinapoongezwa ndani ya kitenzi au mwishoni mwa kitenzi, vinawakilisha au vinasimama badala ya majina, km.
-ye = mtu;  -cho = kitu;  -lo = jambo;  -po = mahali,      ...

(iii)     Viwakilishi vya kurejesha ni chombo muhimu cha       kuundia aina moja ya tungo ambazo huitwa vishazi-tegemezi.

(d)       Viwakilishi vya Nafsi, huwakilishwa na:
 (i)       Viwakilishi-Nafsi huru: mimi ~ sisi; wewe ~ nyinyi; yeye ~ wao.
Maneno haya yote husimama peke yake, na yenye maana kamili yakiwa mazima hivo hivo kwa kujitosheleza. Wala hayajiambatanishi kwenye maneno katika lugha; ni maneno huru kabisa.                       


(ii)       Viwakilishi-nafsi viambata: huwakilishwa na: ni- ~ tu-; u- ~ m-; a ~ wa.katika:
                        ni- ó mimi;  u- ó wewe
                        tu- ó sisi;     m- ó ninyi/nyinyi
                        a- ó yeye      wa ówao

Zingatia:
 (iii)    Viwakilishi hivi huitwa viambata kwa sababu hufungwa mbele ya kitenzi:
ni (na) soma u (na) soma   
tu (na) soma  m (na) soma
a (na) soma    wa (na) soma

 (iv)     Viwakilishi viambata hivi vikisimama peke yake, hufanya kazi ya neno, kwa mfano:
                        (a)       Mimi ni mzima. (ii) Wewe u mzima.       
(b)       Sisi tu wazima.

 (v)      Viwakilishi-nafsi rejeshi: huwakilishwa na: {-ji-}, {-ye-} kama vile:
(a)  Nina-ji-kosoa = Mimi naikosoa nafsi yangu           
(b)  Wana-ji-sifu = Wao  wanazisifu nafsi zao
(c)  Mna-ji-dharau= Ninyi mnazidharau nafsi zenu                                                     
.                                  
        (vi)          Viwakilishi vya kumiliki au viwakilishi vimilikishi ni kama ifuatavyo:
                                                                                               
            Umoja         Wingi   
            -angu              -etu
            -ako                -enu
            -ake                -ao

                                             
                                     Vitenzi (T)

Vitenzi ni maneno yanayoarifu jambo ambalo hufanywa na jina au kufanyiwa jina,  kiwakilishi au kivumishi kinaposimama peke yake kama jina.

Vitenzi hutaja:
(i)        matendo, kama vile: Mwalimu anachora.
(ii)       matukio, kama vile: Simba amejificha porini.
(iii)     mabadiliko, kama vile: Jamila amekua

Katika Kiswahili, kitenzi ni neno linalobebeshwa vipashio vingi ndani yake. Kwa sababu hii, wanaisimu hupendelea kuliita neno hili ‘kifungu-tenzi’ na kukipa alama {fT} badala ya kuliita tu kitenzi kwa alama {T}. Ieleweke tu kwamba alama zote hizi mbili hutumika kwa maana sawa.                                   

                                        
                                                      Vielezi (E)

Vielezi ni maneno au vifungu vya maneno ambavyo kwa pamoja huelezea zaidi tendo au kivumishi.
           
Kuelezea zaidi tendo, kwa mfano:           
 (i)       namna gani (vipi), kama vile: Anakula wima.
(ii)       mara ngapi, kama vile: Dada anaoga mara mbili kwa siku.
(iii)     kiasi gani
(iv)      wapi
(v)       lini
(vi)      kwa sababu gani
(vii)    katika mazingira gani, nk.

Kuelezea zaidi kivumishi, kwa mfano:
(i)                 (Mtu) mnene sana.
(ii)             (Mtu) mnene kupita kiasi. nk.
           

                                               Viunganishi (U)

Viunganishi (U) ni maneno au viambishi vinavyounganisha pamoja jina na jina au tungo na tungo. Kuna aina mbili ya viunganishi:

(a)    Vihusishi, kama vilivyooneshwa katika  sentensi zifuatazo:
(i)     Asys na Mbaraka wamefika.
(ii)    Wamekuja pamoja na mjomba.
(iii)  Alifyeka dimba lakini hakulima.
(iv)   Nilichungulia wala sikumwona.
(ii)       Tumekuja kwa sababu tuna shida na wewe.
(iii)     Tulimkuta analima na kupanda.                                                         

(a)        Vitegemezi (viambishi), kama vilivyooneshwa katika  sentensi zifuatazo:
(i)     Alipofika nyumbani, hakunikuta.
(ii)    Juma aliendelea tu kubisha ijapokuwa alikatazwa.
(iii)  Mbaraka alizawadiwa kwa sababu amefaulu mtihani.


                                                    
                                                            Vihisishi (H)

Vihisishi (H) ni maneno yanayodokeza vionjo vya moyo, kama vile: furaha, huzuni, uchungu, mshangao au mshituko, huruma au laana, matumaini au kukata tamaa, nk.

Aghalabu, vihisishi ni maneno ya mkato, na yafuatayo ni baadhi yake: 
aa!                   asante!                       ee!                   vizuri!                                   
hata!               basi!                           simile!            ewa!               
barabara!       nini!                            zii!                  sawa!
ajabu!             nani!                           kumbe!           lo!
hodi!               sasa!                           pole!               hebu!             
afanaleki!      ati (eti)!                      karibu!           tena!                                      
ebo!                la hasha!                    vema!             Je!                                                                   lahaula!
                                                               
Kwa mfano:
(i)        Lo!, kasema nini huyu!
(ii)       Barabara! Nenda Bwana; haraka!


jiunge nasi bofya hapa ku-install application yetu swahiliform ili usisumbuke kuingia kwenye website yetu



MAREJEO



Maganga (1997), OSW 102: Historia ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.
Masebo, J. A. Nyengwine, N. (2002), Nadharia ya Lugha ya Kiswahili, Kidato cha 5 na 6.  Aroplus Industries Ltd: Dar es Salaam.
Nkwera, Fr. F. V. (2003), Sarufi, Fasihi na Uandishi wa Vitabu, Sekondari na Vyuo. Creative Prints Ltd: Dar es Salaam.



Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

3 comments:

  1. Asante kwa somo hili ambalo ni nzuri sana kwa Kiingereza linaitwa PARTS OF SPEECH

    ReplyDelete