MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UANDIKAJI WA KUMBUKUMBU ZA MKUTANO.




a)KICHWA CHA KUMBUKUMBU 

Kichwa cha kumbukumbu kitaeleza mkutano unahusu nini, mahali ulipofanyika na tarehe ya 

kufanyika kwake, huandikwa kwa herufi kubwa. Mfano “KUMBUKUMBU YA MKUTANO 

WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE KILICHOFANYIKA TAREHE 05/04/2018 

KATIKA UKUMBI WA SHULE KUANZIA SAA 4:00-6:00 MCHANA. 

b)MAHUDHURIO 

Mwandishi anapaswa kuandika orodha ya majina yote waliofika kwenye mkutano kulingana na 

vyeo vyao kwa kuanzia na yule mwenye cheo cha juu zaidi hadi kwa wanachama. Pia 

wasiohudhuria waandikwe majina yao wale waliotoa hudhuru na wasiotoa hudhuru. 

c)AJENDA

Mwandishi anapaswa kuandika ajenda au mambo yatakayozungumzwa katika mkutano. Mambo 

yaliyojadiliwa yaandikwa kwa muhatasari na kauli ya kukataliwa au kukubaliwa iandikwe 

waziwazi 

d)KUFUNGUA MKUTANO 

Mwenyekiti akishafungua mkutano, mwandishi au Katibu aandike saa ya kufungua mkutano na 

muhtasari wa yaliyozungumzwa 

e)KUFUNGA MKUTANO 

Baada ya majadiliano ya ajenda, mwenyekiti afunge mkutano. Mwandishi/Katibu azingatie muda wa kufungwa kwa mkutano. 

MFANO WA KUMBUKUMBU ZA MKUTANO ULIOFANYIKA MARA YA KWANZA 

KUMBUKUMBU ZA MKUTANO WA CHAMA CHA KISWAHILI ULIOFANYIKA 

KATIKA CHUMBA CHA MIJADALA TAREHE 13/06/ 2017 KUANZIA SAA TATU 

ASUBUHI 

1.MAHUDHURIO 

Waliohudhuria ni wajumbe watano (03) na wasiohudhuria ni wajumbe watatu (03): 

Waliohudhuria 

i.Kapalata Hussein  Mwenyekiti 

ii.Vaileth Mpagama – Mweka hazina 

iii.Meta Mkorofi  katibu 

Wasiohudhuria 

i.Chinguwile Said – Naibu Mwenyekiti (Safarini) 

ii.Ponea Kamgazi  Msimamizi wa Mijadala (udhuru) 

iii.Juma Alex (hakuna taarifa) 

2.AJENDA 

i.Kufungua Mkutano 

ii.Uchapishaji wa jarida la Kiswahili 

iii.Mengineyo 

iv.Kufunga mkutano 

3.KUFUNGULIWA KWA MKUTANO 

Mwenyekiti alifungua mkutano mnamo saa 10:30 alasiri kwa kuwakaribisha wajumbe wote. 

4.UCHAPISHAJI WA JARIDA LA KISWAHILI 

Wanachama walikubaliana, Kwamba chama kitaanza kuchapisha jarida la Kiswahilina litakuwa 

likichapishwa mara moja kila muhula na kuuzwa shuleni. Na kila mwanachama atachangia 

katika kuandika makala na kuuza nakala za jarida hilo. 

5.MENGINEYO 

Wajumbe walisisitiza sana kwamba kamati iwajibike ipasavyo kuhakikisha jarida linatoka kwa 

haraka 

.KUFUNGA MKUTANO 

Mwenyekiti alifunga mkutano kwa kuwaomba wajumbe watoe ushirikiano katika uongozi ili 

jarida lifanikiwe haraka iwezekanavyo. Mkutano ulifungwa saa 12:00 jioni 

Mwenyekiti…………….…… Katibu…….………………………

Sahihi……………………………… Sahihi………………………

Tarehe………………....……………. Tarehe…………………………

•Ikiwa mkutano unafanywa kwa mara ya pili au zaidi, mwandishi/Katibu hana budi 

kuzingatia vipengele vifutavyo: 

a.KUSOMA NA KUTHIBITISHA KUMBUKUMBU 

Baada ya kufungua mkutano, kumbukumbu za mkutano uliopita zinapaswa kusomwa na 

kuthibitishwa kwamba ni za kweli kisha Mwenyekiti na Katibu wanapaswa kutia saini 

b.YATOKANAYO NA KUMBUKUMBU 

Yatokanayo na kumbukumbu ni yale mambo yote yaliyojadiliwa kutoka mkutano uliopita. Baada 

ya kusoma na kuthibitisha kumbukumbu wajumbe hujadili kuhusu yale yaliyoamuliwa 

kutekelezwa. Majadiliano kuhusu yatokanayo yakishafanywa na maoni na mapendekezo 

yakatolewa mwandishi hufikia hatua ya kufunga mkutano kama tulivyoona katika kumbukumbu 

za mkutano wa mara ya kwanza. 



Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment