DHIMA YA FASIHI SIMULIZI


(a)        Kuelimisha. 
         Dhima hii inatokana na ukweli kuwa kuna maudhui yenye upana katika kazi hizo andishi; aghalabu umuhimu wa fasihi andishi katika kuelimisha hujitokeza kwenye taasisi za elimu: shuleni, vyuoni, nk..

(b)        Kuburudisha.       
         Ziko kazi zinazoburudisha ambazo ni za tanzu zote tatu.

(c)        Kuadhibu na kunasihi jamii. 
         Mara nyingi kazi hizo za fasihi andishi hutumika katika kuasa na kuadhibu juu ya mambo mbali mbali yanayojitokeza katika jamii.

(d)        Kutia hamasa, kwa upande wa ushairi na kumfanya mtu asikate tamaa
         Kwa mfano, Kandoro(1972:138-155) aliwahi kuelezea hamasa ya wananchi waliokuwa wameungana kama “Siafu Wamekazana”. Tunamwona pia mwandishi kwa hamasa akiwaita “Waafrika Njooni” au “Kwetu ni Kwao kwa Nini?” Tunaona wazi kuwa kazi hizo zinajitahidi kuendeleza mapambano dhidi ya ukoloni mkongwe na mamboleo.

(e)        Kupiga vita kwa hali na mali mazingira yote ya ujinga, maradhi, njaa na umaskini.
          Katika kuthibitisha hoja hii kwa mfano, tuna tamthilia kama vile Hawala ya Fedha ambayo inapambana na maovu kama uvivu, kutojua kusoma na kuandika na mengineyo. Au tamthilia kama vile Ngoswe inayojadili na kupiga vita uzembe, uvivu na mengineyo. Kimsingi ndivyo ilivyo katika tanzu nyingine za fasihi andishi.


Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment