Aina za Viambishi




Ziko aina kuu tatu za viambishi vinavyonatishwa kwenye mzizi, nazo ni:
                       
(i)        Viambishi vya Mwanzoni  mwa  Mzizi
Kati ya hivi Viambishi vya mwanzoni mwanzoni mwa mzizi, kuna:

(a)       kile cha kwanza kabisa ambacho kiko mbali na mzizi ambacho hujulikana ama Kiambishi-Ngeli, au  Kiambishi cha Idadi, au Kiambishi Nafsi (mtenda, mtendwa au  mtendewa).

(b)       kile cha kwanza kabisa kinachogusana na mzizi.

(c)       kile kilichoko/vile vilivyoko kati ya kile cha kwanza kabisa  ambacho kiko mbali na mzizi na kile cha kwanza kabisa kinachogusana na mzizi.
                       
Kwa mfano, katika neno tutampiganisha (= tu-ta-m -pig - an-ish-a) :
·        tu-ta-m- ni viambishi vya mwanzoni mwanzoni mwa mzizi, -pig-.

·        tu- ni kiambishi cha kwanza kabisa ambacho kiko mbali na mzizi, -pig-, (mtenda).
·        -m- ni kiambishi cha kwanza kabisa kinachogusana na mzizi, -pig-, (mtendwa).

(d)       -ta- ni kiambishi kilichoko kati ya kile cha kwanza kabisa ambacho kiko mbali na mzizi na kile cha kwanza kabisa kinachogusana na mzizi, -pig-, (njeo ijayo).
                       
(ii)       Viambishi vya Mwishoni mwa Mzizi
Kati ya hivi Viambishi vya mwishoni mwa mzizi, kuna:

(a)       kile cha mwisho kabisa ambacho kiko mbali na mzizi na ambacho aghalabu huitwa kiambishi tamatishi.      
           
(b)       kile cha mwisho, lakini cha kwanza kugusana na mzizi.

(c)       kile kilichoko/vilivyoko kati ya kile cha mwisho kabisa ambacho kiko mbali na mzizi na kile cha mwisho, lakini cha kwanza kugusana na mzizi.
                       
Kwa mfano, katika neno tutampiganisha (tu-ta-m -pig - an-ish-a)                 
·        -an-ish-a ni viambishi vya mwishoni mwishoni mwa mzizi, -pig-.

·        -a ni kiambishi cha mwisho kabisa ambacho kiko mbali na mzizi, -pig-, (kiyakinishi cha kauli).

·        -an- ni kiambishi cha kwanza kabisa kinachogusana na mzizi, -pig-, (kitendeana cha kauli).

·        -ish- ni kiambishi kilichoko kati ya kile cha mwisho kabisa [a} ambacho kiko mbali na mzizi na kile cha kwanza kabisa {an} kinachogusana na mzizi, -pig-, (kitendea cha kauli).


Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment