Kiswahili kiliingizwa nchini Burundi na Wajerumani mara walipoanza kutawala Tanganyika, Rwanda na Burundi kwa miaka thelethini (30) yaani (1885 – 1916).
1 Wakati wa
Utawala wa Wajerumani (1885 – 1916)
Mnamo mwishoni mwa karne ya 19, ndipo Kiswahili kilianza kuingia nchini
Rwanda wakati wa utawala wa Wajerumani. Wajerumani waliwachukua baadhi ya
watumishi wao kutoka Tanganyika ambako idadi kubwa ya watu walikuwa
wakizungumza Kiswahili na kuja nao mpaka Rwanda kufanya kazi. Na katika kipindi
hicho, ndipo Kiswahili kilianza kuingia nchini Rwanda na kuanza pole pole
kupata wazungumzaji.
2 Wakati wa Utawala wa Wabelgiji (1945 -1960)
Baada ya Wajerumani
kushindwa katika Vita ya Kwanza ya Dunia (1945), nchi ya Burundi na Rwanda
ziliwekwa chini ya Himaya ya Ubelgiji.
Wakati wa utawala wa
Wabelgiji, kuenea kwa Kiswahili nchini Burundi kulikumbwa na matatizo mengi.
3 Mbinu za
Wabelgiji za Kukidunisha Kiswahili Nchini Burundi
Aghalabu watawala
hao wa kibelgiji badala ya kikiendeleza Kiswahili, walikuwa wakitafuta mbinu
kadhaa na kuzitumia kukidunisha Kiswahili nchini Burundi ili kisiendelee kama
ifuatavyo:
(a) Dharau - lugha ya Kiswahili haikutiliwa mkazo waliouanzisha Wajerumani;
mafunzo ya Kiswahili yalipungua sana; waliidharau.
(b) Wabelgiji
walitilia mkazo zaidi mafunzo ya lugha ya Kifaransa na Kiflemishi badala ya
Kiswahili.
(c) Waarabu wa mji wa Bujumbura, watumwa na
wafuasi wao tu, yaani wenyeji wa Kiafrika (Wabantu) ndio waliokizungumza
Kiswahili, tena majumbani mwao tu.
(d) Udini
nao ulikuwa sababu kubwa ya kukidunisha Kiswahili huko Burundi. Kwa kuwa
Wabeligiji walikuwa ni Wakristo, kwa upande mmoja, na kwa upande mwengine,
Waarabu wa mji wa Bujumbura, baadhi ya watumwa na wafuasi wao ni Waislamu,
hivyo Kiswahili kilizuiliwa kisienee, kwani Wabelgiji waliwachukia Waarabu na
Waislamu kwa ujumla.
4 Juhudi za
Kukuza Lugha ya Kiswahili Nchini Burundi
Juhudi kubwa za
kuikuza lugha ya Kiswahili nchini Burundi zilianza kuonekana hasa tangu mwaka
1963 ambapo hatua madhubuti zilichukuliwa na Serikali kama ifuatavyo:
(a) Habari za ‘vipindi vya salamu’ mbalimbali vilianza kusikika
katika Redio Burundi.
(b) Serikali iliingilia kati na kuwataka wananchi wazungumze
Kiswahili.
(c) Serikali iliamua Kiswahili kianze kufundishwa vyuoni, kwa kuanza
na Chuo cha Wanajeshi cha Bujumbura, mwaka 1965, na baadaye Chuo Kikuu cha
Bujumbura.
(d) Katika Taasisi ya mabwana fedha, taasisi ya mawasiliano ya simu,
Kiswahili kilifundishwa vile vile.
(e) Kwa mujibu wa maelezo ya Halid Hassan, katika Maganga (1997:1600), Wakimbizi wa ki-Rundi
waliokimbilia Tanzania mnamo mwaka 1970 na baada ya miaka kadhaa kurejea tena
makwao Burundi wameonesha kuwa na umilisi mkubwa wa lugha ya Kiswahili.
Asante kwa hii habari. Tafadhali tueleze hali ya lugha ya Kiswahili ilivyo sasa nchini Burundi.
ReplyDelete