VIKWAZO VYA KUJIFUNZA LUGHA YA KISWAHILI



VIKWAZO VYA KUJIFUNZA LUGHA YA KISWAHILI

  • ·         KUWEPO KWA LUGHA MAMA:

Lugha mama au  lugha ya kwanza au kama tulivyozoea lugha ya kikabila huleteleza matatizo katika ujifunzaji wa kiswahili kwa wanafunzi. Tatizo kubwa linalosababisha na lugha mama ni tatizo la kimatamshi ambalo huweza pia kupelekea tatizo la kimaandishi. Kwa mfano unaweza kusikia mtu akitamka fyatu badala ya viatu.


  • ·         KASORO ZA KIMAUMBILE.

Athari za kimaumbile au kasoro za kimaumbile huweza kusababisha vikwazo katika utamkaji wa maneno ya kiswahili kwakuwa kunakuwepo na matatizo katika mfumo wa ala za sauti za mtamkaji ai mjifunzaji. Kwa mfano mtu mwenye kithembe hutumia sauti th badala ya s.
Vilevile kuna magonjwa ambayo huweza kumfanya mtu kushindwa kutamka baadhi ya maneno kwa usahihi  kama vile kiharusi.


  • ·         KUWEPO KWA LUGHA ZA KIGENI.

Kuwepo kwa lugha kigeni katika nchi yetu mfano kingereza , kifaransa. Huchangia kwa kiasi kikubwa kuharibu matamshi ya kiswahili sanifu kutokana na athari za lugha hizo kwa watanzania wengi. Hali hii husababisha matatizo katika hatua za ujifunzaji wa lugha ya kiswahili kwa watu wengi.



Share on Google Plus

About Se

mwiza peter ni mwalimu ambaye alipata taaluma hii chuo cha ualimu morogoro(motco) kwa sasa nipo mwanza Tanzania ni miongoni mwa vijana ambao lengo langu nikukufanya wewe kupata elimu kuhusu somo la kiswahili na kuongeza ufaulu wa somo hili. tupo mwanza Tanzania.karibu mwaa tunawapenda wote.elimu ni ukombozi wa maisha chukua hatua
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment